Superstar wa Bongo movie Wema Isaac Sepetu aka Beutiful Onyinye hivi karibuni
alimuharibia siku Emanuel Myamba maarufu kama Pastor Muyamba, kwa
kushindwa kufika kwenye hafla iliyokuwa imeandaliwa na chuo chake cha
sanaa ‘TFTC’ akiwa kama mgeni rasmi.
Wema Sepetu.
Mtoa habari wetu ndani ya taasisi hiyo aliliambia gazeti hili kuwa,
Wema aliombwa na kukubali kuhudhuria shughuli hiyo, lakini alipopigiwa
simu dakika za mwisho aliwaambia kwamba atashindwa kufika kwa kuwa
amefiwa na shangazi yake udhuru ambao baadaye ulibainika kuwa haukuwa wa
kweli